Skip to main content
- Watu wote wa Mungu, njooni tumwimbie,
Yesu Mwokozi wetu, alituokoa.
Alikufa mtini, kwa ajili yetu,
Makosa yetu yote, aliyachukua,
Alituweka huru, kwa mauti yake.
- Tushike Neno lake, tuwe na imani,
Tukeshe kwa kuomba, Yesu atarudi.
Tusiyasumbukie, ya ulimwenguni.
Ulevi na ulafi, tusiyarudie,
Ili tuwe tayari, kwa siku ya Bwana.
- Ni siku ya furaha, tukiwa tayari,
Tutakapokutana, huko mawinguni.
Atatukaribisha, kwake mbinguni juu,
Tutakuwa pamoja, na Mwokozi wetu,
Na Mungu Baba yetu, aliyetupenda.
- Sasa wakati wetu, tufanye haraka,
Kueneza Injili, watu waokoke.
Mavuno mengi kweli, twende tukavune.
Mapenzi yake Bwana, tuwe waaminifu.
Ujira tutapewa, taji ya uzima.
Comments
Post a Comment