1 WATU WOTE WA MUNGU

  1. Watu wote wa Mungu, njooni tumwimbie,
    Yesu Mwokozi wetu, alituokoa.
    Alikufa mtini, kwa ajili yetu,
    Makosa yetu yote, aliyachukua,
    Alituweka huru, kwa mauti yake.


  2. Tushike Neno lake, tuwe na imani,
    Tukeshe kwa kuomba, Yesu atarudi.
    Tusiyasumbukie, ya ulimwenguni.
    Ulevi na ulafi, tusiyarudie,
    Ili tuwe tayari, kwa siku ya Bwana.


  3. Ni siku ya furaha, tukiwa tayari,
    Tutakapokutana, huko mawinguni.
    Atatukaribisha, kwake mbinguni juu,
    Tutakuwa pamoja, na Mwokozi wetu,
    Na Mungu Baba yetu, aliyetupenda.


  4. Sasa wakati wetu, tufanye haraka,
    Kueneza Injili, watu waokoke.
    Mavuno mengi kweli, twende tukavune.
    Mapenzi yake Bwana, tuwe waaminifu.
    Ujira tutapewa, taji ya uzima.

Comments