10 DAMU YAKO YENYE BARAKA

  1. Damu yako yenye baraka, Inayoosha
    makosa, Ilimwagwa m-salabani, Mwokozi
    ulipokufa. Nastahili ’pata hukumu,
    Na siwezi mimi kujiosha. Unioshe katika
    damu, Nipate kuwa safi kweli!


    Safi kabisa! Safi kabisa! Unioshe katika
    damu, Nipate kuwa safi kweli!



  2. Yesu, ulivikwa miiba, Kuangikwa juu ya
    mti, Ulivumilia mateso ’jeraha na
    maumivu. Ninataka kijito hicho, Niende
    nisafishwe kabisa! Unioshe katika damu,
    Nipate kuwa safi kweli!


  3. Baba, kweli nina makosa, Moyo wangu u
    dhaifu; Mimi mwenye dhambi rohoni,
    Nipate wokovu wapi? Yesu, kwako
    m-salabani, Naja ninakuamini sasa,
    Unioshe katika damu, Nipate kuwa safi kweli!


  4. Bwana, nimekukaribia, Nilindwe nawe
    milele! Unifungue kila kamba, Uujaze
    moyo wangu! Na karibu ya m-salaba,
    Nitakaa hata kufa kwangu, Unioshe
    katika damu, Nipate kuwa safi kweli!

Comments