111 MTOTO YESU AMEZALIWA


1. Mtoto Yesu amezaliwa – Bethlehemu! Furahi watu wa Mungu, :/:Haleluya!:/:


2. Bikira alipata nafasi – Horini kumzaa. Kristo duniani. :/:Haleluya! :/:


3. Yesu ’kazaliwa pamoja na – Wanyama. Malaika ’kamwimbia. :/:Haleluya!:/:


4. Na Wachungaji wakamwabudu – Horini. Wakamsifu Bwana Yesu. :/:Haleluya!:/:


5. Twakaribishwa kuwa watoto – wa Mungu, Kukaa naye mbinguni. :/:Haleluya!:/:


6. Na sisi tumepata wokovu – Milele. Mwokozi amezaliwa. :/:Haleluya!:/:

7. Tutamwimbia kwake huko juu – Pamoja Na malaika wa Mungu. :/:Haleluya!:/:


8. Tumshukuru aliyezaliwa – Mwokozi Ndiye ndugu yetu mkuu. :/:Haleluya!:/:


Comments