- Nimekombolewa na Yesu,
Aliyenirehemia,
Kwa bei ya mauti yake,
Nimekuwa mtoto wake
Kombolewa! Nakombolewa na damu.
Kombolewa! Mimi mwana wake kweli. - Kukombolewa nafurahi,
Kupita lugha kutamka,
Kulionyesha pendo lake,
Nimekuwa mtoto wake. - Nitamwona, uzuri wake,
M-falme wangu wa ’jabu.
Na sasa najifurahisha,
Katika neema yake. - Najua taji imewekwa,
Mbinguni tayari kwangu,
Muda kitambo atakuja,
Ili alipo niwepo.
Comments
Post a Comment