133 UFURAHI, MOYO WANGU


1. Ufurahi, moyo wangu, Umepata uheri.
:/:Sikitiko limekwisha, Yesu ni Mwokozi wangu.:/:


2. Ameponya roho yangu, Ni Mganga wa kweli,
:/:Kwa Roho Mtakatifu Abatiza watu wake.:/:


3. Yesu ameliandika, Jina langu mbinguni,
:/:Sasa mimi mali yake Milele hata milele.:/:


4. Na moyoni mwangu sasa Naimba: “Mungu Baba”.
:/:Ni furaha kubwa sana, Nina rafiki kila saa.:/:


5. Nimeondolewa dhambi, Sitarudi tena!
:/:Kweli Yesu aokoa,Wenye dhambi Kila siku.:/:


6. Nyimbo za kumsifu Mungu Zinavuma Mbinguni,
:/:Nami pia ninaimba: “Mungu Wangu usifiwe!”:/:


Comments