15 MUNGU WASHA MOTO

  1. Mungu, washa moto wako kwangu,
    Ninangoja nguvu yako. Nipe uzima na
    pendo lako, Unijaze, ee Mwokozi wangu!


  2. Teketeza usiyoyapenda, unisafishe
    kwa damu. Na kiburi changu ukivunje,
    Unioshe Yesu, niwe safi!


  3. Unilinde Yesu, nisiasi, Unifunge
    kwa upendo. Mimi ni dhaifu, unitunze,
    Niongoze kwa m-kono wako!


  4. Huko mbinguni tutafurahi, Na huzuni
    zitakwisha. Nyimbo zitaimbwa za kusifu;
    Utukuzwe, Yesu, Mkombozi!

Comments