- Ukae nami, giza lafika! Usiniache, Mungu, Naomba! Unajua udhaifu wangu. Nakutegemea, Uwe nami!
- Maisha yangu mafupi sana. Uzuri wa dunia wapita. Kuna machozi na kufa pia. Mkombozi wangu, Uwe nami!
- Nakuhitaji wewe daima, Una uwezo wa kunilinda. Wewe shujaa wa kushinda wote, Kati’ hali zote, Uwe nami!
- Nionyeshe m-salaba wako, Nione nuru yako gizani. Na nikiishi, hata nikifa. Mkombozi wangu, Uwe nami!
Comments
Post a Comment