18. MUNGU WETU YU KARIBU

  1. Mungu wetu yu karibu, Kutupa nguvu
    zake. Mbingu ina maghubari,
    Tuletee mvua sasa.


    Tusikie Mungu wetu, Tubariki saa hii!
    Tunangoja, tunangoja, Kujazwa nguvu zako.



  2. Mungu wetu yu karibu, Hapa patakatifu.
    Sisi sote tunangoja, Kujazwa naye Mungu.


  3. Mungu wetu yu karibu, Kwa imani
    twaomba,“Tuwashie moto safi, Ndani ya
    roho zetu!”


  4. Mungu, ufungue mbingu, Twaomba nguvu
    zako. Utubarikie sasa, Kwa rehema yako kuu!

Comments