1. Ndugu tufanye kazi, siku zinapita!
Tumtumikie Mungu kwa nguvu zote!
Tuanze asubuhi na tuendelee!
Mbio usiku waja, Kazi ’takwisha.
2. Ndugu tufanye kazi, tungali wazima!
Tusipoteze bure nafasi zetu!
Tuyatimize yote bila kukawia!
Mbio usiku waja, Kazi ’takwisha.
3. Ndugu tufanye kazi, mapenzi ya Mungu!
Katika kuhubiri tuwe na bidii!
Tumtumikie Mungu kwa uwezo wote!
Mbio usiku waja, kazi ’takwisha.
Comments
Post a Comment