- Mungu tunangoja wote, Roho M-takatifu, Tunaomba kwa imani, Umtume hapa kwetu
Mungu wetu, Umimine Roho yako juu yetu! Mioyoni mwetu, Bwana, Timiza kazi yako! - Washa moto wako tena, Ndani ya roho zetu, Hata vyote vya majani, Viteketeze Bwana!
- Utakase roho zetu, Na kiburi kivunje, Wewe u M-falme wetu, Tawala watu wako!
- Utujaze siku zote, Pendo lako ee Mungu! Sisi tuwe nyumba yake, Roho M-takatifu!
- Na karama zake Roho, Utugawie zote! Na wagonjwa uwaponye, Wote wakutukuze!
Comments
Post a Comment