19 MUNGU TUNANGOJA WOTE

  1. Mungu tunangoja wote, Roho M-takatifu, Tunaomba kwa imani, Umtume hapa kwetu


    Mungu wetu, Umimine Roho yako juu yetu! Mioyoni mwetu, Bwana, Timiza kazi yako!


  2. Washa moto wako tena, Ndani ya roho zetu, Hata vyote vya majani, Viteketeze Bwana!


  3. Utakase roho zetu, Na kiburi kivunje, Wewe u M-falme wetu, Tawala watu wako!


  4. Utujaze siku zote, Pendo lako ee Mungu! Sisi tuwe nyumba yake, Roho M-takatifu!


  5. Na karama zake Roho, Utugawie zote! Na wagonjwa uwaponye, Wote wakutukuze!

Comments