- Bwana Yesu niongoze, Salama baharini,
Juu ya mawimbi mengi, Na katika dhoruba!
Bwana Yesu niongoze, Ninakutegemea! - Bwana Yesu, niongoze, Unitulize moyo!
Sema neno moja tu, Patakuwa shwari kuu.
Bwana Yesu niongoze, Unipe utulivu! - Bwana Yesu, niongoze, Nishinde majaribu!
Mengi yanidanganya, Na kunifumba macho!
Bwana Yesu niongoze, Niwe mshindi kweli! - Bwana Yesu, niongoze, Hata nivuke ng’ambo!
Na nikiona giza, Nipe nuru na raha! Bwana
Yesu niongoze, Uwe nami milele.
Comments
Post a Comment