207 UMGEUKIE MWOKOZI

1. Umgeukie Mwokozi Na ujitenge na dhambi!
:/:Babako angoja ufike Ili usiangamie!:/:


2. Kijana, unafurahia Anasa za ulimwengu.
:/:Baada ya muda kitambo Nawe utahukumiwa.:/:


3. Kwa nini kujiangamiza Kwa kufuata dunia.
:/:Usijipoteze dhambini Na kukosa tumaini.:/:


4. Umkimbilie Mwokozi, Naye atakupokea.
:/:Na utaokoka hakika Kwa nguvu ya damu yake!:/:


5. Walio mbinguni waimba, Wenye mavazi meupe.
:/:Hutaki kukaa pamoja Na watu wa Baba Mungu?:/:


6. Je, mwisho utaona wapi Mahali pa kujificha?
:/:Dunia itakapochomwa Utakosa kimbilio.:/:


7. Ujipatanishe na Mungu, Rafiki usichelewe!
:/:Ukimkataa Mwokozi, Utapotea milele.:/:


8. Chagua bila kukawia! Yesu atakupokea.
:/:Angoja ufike kutubu, Apate kukuokoa.:/:


Comments