1. Hatumjui Rafiki mwema, Ni Bwana Yesu tu.
Yeye mwenyewe atufahamu, Yesu peke yake
Yesu anatujua kweli, Njia anatuonyesha.
Yesu Rafiki kupita wote, Wote wa dunia.
2. Hakuna rafiki kama Yesu, Hakuna, hakuna!
Na pendo lake ni la ajabu, Ladumu milele.
3. Je, ataweza kutusahau? Hawezi, hawezi!
Twafarijiwa kwa pendo lake Kila saa, kila saa.
4. Je, amevunja agano lake? Hapana, hapana!
Je, alim-fukuza yeyote? Hakuna kabisa!
5. Nani Rafiki mpendwa wangu? Ni Bwana Yesu tu.
Anastahili kupata sifa Huku na mbinguni.
Comments
Post a Comment