22 YESU U RAFIKI YANGU

  1. Yesu u rafiki yangu, Una uwezo kweli,
    Wa kuziondoa dhambi, Na kutakasa roho.


    Ninaomba masamaha, Nipe ushindi wako,
    Unilinde hata mwisho, Unitwae kwako juu.



  2. Mimi nilikuwa mwovu, Sikukupenda Yesu
    Kwa hakika sikujua, Wewe na pendo lako.


  3. Bwana Yesu usamehe, Dhambi nilizofanya
    Nisishindwe na jaribu, ’nijaze nguvu zako!


  4. Tangu sasa wewe Yesu, U Mkombozi wangu,
    Niwe mbali na Shetani, Niwe wako daima!

Comments