232 NILIPOFIKA KWA MWOKOZI

1. Nilipofika kwa Mwokozi, Nikapaza sauti yangu
“Yesu Bwana, unirehemu! Uniokoe!”


Sifa kwa Yesu, Mwokozi wangu!
Alisikia ombi langu, Sifa kwa Yesu!


2. Nilipofika msalabani, Nikamsihi Bwana Yesu:
“Unitakase, niwe safi.” Akasikia!


3. Chemchemi ya msalabani Hata leo yabubujika,
Kuokoa na kusafisha Wakati wote.


4. Njoo kwa Yesu hata wewe, Unywe, uoshwe moyo
wako: Kiu ipoe, utakaswe, Umsifu Yesu!

Comments