235 TUMEOKOKA TOKA DHAMBI

1. Tumeokoka toka dhambi, Usikilize, ee rafiki!
:/:Tumeokoka tufike juu, Kuvikwa taji. Furaha
kuu!:/:


2. Tumeokoka, tu salama, Wakitucheka - ni kwa
muda! :/:Twavumilia shida zote Twatazamia heri
kule!:/:


3. Tumeokoka, tuko huru, Tukichokozwa haidhuru.
:/:Tutaiacha dunia hii Na kukaribishwa
mbinguni!:/:


4. Tumeokoka. Furaha kuu! Twaandaliwa karamu
Juu! :/:Salamu hiyo utangaze, hata wengine
Waokoke!:/:


5. Kwani kungoja Mama, Baba? Twende pamoja
Ndugu, Dada! :/:Hataingia asitaye. Yesu akwita:
Leo uje!:/:



Comments