- . Ee Mungu mwenye kweli, Ninakuamini.
Maneno yako yote, Yadumu milele.
“Nitakusaidia wakati uitapo!”
Bwana, nategemea ahadi yako hii. - Na katika uchungu Heri kuamini,
Ninajitoa kwako, Baba, unilinde.
Uliyenifundisha Kuita jina lako,
Naona tumaini, tena tegemeo. - Yote ninayoomba Unayasikia,
Yaliyo mema kwangu najua wafanya.
Katika shida zote waweza kunilinda,
Unanisaidia na kunituliza.
Comments
Post a Comment