24 EE MUNGU MWENYE KWELI

  1. . Ee Mungu mwenye kweli, Ninakuamini.
    Maneno yako yote, Yadumu milele.
    “Nitakusaidia wakati uitapo!”
    Bwana, nategemea ahadi yako hii.


  2. Na katika uchungu Heri kuamini,
    Ninajitoa kwako, Baba, unilinde.
    Uliyenifundisha Kuita jina lako,
    Naona tumaini, tena tegemeo.


  3. Yote ninayoomba Unayasikia,
    Yaliyo mema kwangu najua wafanya.
    Katika shida zote waweza kunilinda,
    Unanisaidia na kunituliza.

Comments