1. Fikiri siku tutakapofika Mbinguni huko juu,
Kwa furaha malaika Watatupokea.
Wataimba wimbo wa kutulaki:
“Karibu! Karibuni mbinguni!” Malaika
wa Mungu wataimba, Wimbo wa furaha:
“Karibuni, Karibuni!”
2. Wapendwa waliotutangulia, Sasa wako kule,
Hawachoki kumsifu, Usiku na mchana.
3. Fikiri tutakapokusanyika, Kwa mto wa uzima,
Kundi kubwa la mbinguni, Litatupokea.
4. Yesu Mwokozi atatupokea, Tena kwa furaha.
Atatukumbatia na kutukaribisha.
Comments
Post a Comment