27 UNA UHODARI LEO

  1. Una uhodari leo, Kumfuata Mwokozi,
    Hata ukichekwa sana, Na kupata mateso?


  2. Una uhodari leo, Kuwa mtu wa Mungu,
    Ukiona haya sasa, Mwisho itakuwaje?


  3. Mji unaonekana Ukiwa mlimani,
    Hivyo na imani yetu, Ionekane wazi.


  4. Ukimpenda Yesu sana Kuliko vitu vyote,
    U tayari kum-kiri, Mbele ya watu wote.


  5. Chuki au pendeleo Yote ni bure kwako,
    Watafuta siku zote, Sifa za Yesu Kristo.


  6. Ujihoji nafsi yako Ukitaka wokovu,
    Uliyem-kana Yesu, Utubu dhambi zako!


  7. Umsihi masamaha, Akuoshe kwa damu,
    Omba uhodari sasa, Kumfuata Mwokozi!


  8. M-chague Yesu leo, M-fuate daima,
    Ukitwaa msalaba, Utapokea taji!

Comments