271 NINASHIKWA NA KIU

1. Ninashikwa na kiu, Bwana, unipe maji,
maji ya uhai ndani ya maisha yangu.


:/: Bwana, Bwana, Yesu Mfalme wangu!:/:


2. Moyo wangu wakupenda, Bwana
Mungu wangu. Nitakuja lini kwako,
Bwana Mfalme wangu?


3. Mchana na usiku Bwana nakulilia. Watu
Wanasema: “Mungu wako yuko wapi?”


4. Huzuni moyoni mwangu, Bwana Mungu wangu.
Watu wengi wadharau, Mungu ’wasamehe!


5. Twashikamana pamoja 
kwenda juu mbinguni.
Twashukuru, twafurahi kushirikiana.


6. Mwokozi, nguvu zaishaje
 moyoni mwangu?
Unisaidie Bwana, 
nitakushukuru.

Comments