1. Mwokozi alifufuka, Haleluya!
Watu wote mwimbieni, Haleluya!
Imbeni kwa furaha, Haleluya!
Viumbe vyake vyo vyote, Haleluya!
2. Kristo alituokoa, Haleluya!
Akamshinda Shetani, Haleluya!
’Katuokoa gizani, Haleluya!
Kutuingiza nuruni, Haleluya!
3. Makaburi mengi sana, Haleluya!
Yakafunuka kabisa, Haleluya!
Ikashindwa mauti, Haleluya!
Kristo ndiye M-shindaji, Haleluya!
4. Mfalme yu hai mbinguni, Haleluya!
Alitushindisha kufa, Haleluya!
Alileta uzima, Haleluya!
Akaondoa hukumu, Haleluya!
5. Yesu ana utukufu, Haleluya!
Nasi tutaishi naye, Haleluya!
Tutakapofufuka, Haleluya!
Tutafanana na Yesu, Haleluya!
6. M-falme wa ulimwengu, Haleluya!
Njoni tumhimidi sote, Haleluya!
Tumwabudu Mwokozi, Haleluya!
Ndiye ufufuo wetu, Haleluya!
Comments
Post a Comment