Skip to main content
28 NAPENDA NIKUFUATE WEWE
- Napenda nikufuate wewe, Yesu daima,
Nikiwa katika shida, dhiki au furaha,
Unaponitangulia, Ninakuja nyuma mbio,
Ninajua ni karibu, Kuwasili kwako juu.
- Haifai niulize, Bwana waenda wapi?
Au kwa kusitasita, Kushika njia yako.
Kweli hapa kazi moja, Ni kukufuata Bwana,
Kwenda njia ile moja, Unayonionyesha.
- . Ukiona kitu tena, Chataka kunifunga,
Au kuwa mgogoro, Katika njia yangu,
Kata kamba mara moja, Ifungayo roho yangu!
Ninataka kuwa huru, Na kukutumikia.
- Bwana Yesu unilinde! Hifadhi nia yangu!
Nikichoka kwa safari, Nong’oneza kwa pendo:
“Mwana u mtoto wangu, Uniandamie punde,
Utapumzika sana, Tena kwangu huko juu!”
Comments
Post a Comment