1. Jina lake Yesu Kristo Lina nguvu daima.
Jina hilo la ajabu litadumu milele.
Linafaa kwa watu wote, Wazee na vijana.
Linaweza kuongoza Kila mtu kwa Mungu.
Jina hilo nalipenda, Lawasha moyo wangu,
Na kwa jina hilo jema, Nimepata wokovu.
2. Jina hilo linavuma Po pote duniani,
Na kwa wote linaleta, Raha na tumaini,
Jina hilo laondoa machukio moyoni,
Ndipo milki ya Mwokozi, Itapata nafasi.
3. Na katika giza huku, Jina hilo linang’aa,
Laonyesha msafiri, Njia yenye uzima.
Jua likitiwa giza, Jina hilo ladumu,
Na milele lisifiwe, Hapa na mbinguni juu.
Comments
Post a Comment