286 ARUSINI HUKO KANA

1. Arusini huko Kana Yesu alialikwa,
Hapo ikaonekana Ishara ya ajabu.


Ushushe Baraka zako Ju-u ya ndugu hawa,
Bwana na Bibi-arusi. Uwaongoze vema.


2. Leo tunakuhitaji Uwe pamoja nao,
Bwana na Bibi-arusi. Ndoa ibarikiwe


3. Yesu U mlinzi wao, Uwalinde taabuni.
Uhifadhi nyumba yao, Waishi kwa amani.


4. Katika raha na taabu Wafungane kwa
pendo, Watumike kwa furaha Mpaka
siku ya mwisho.

Comments