Skip to main content
- Mbinguni ninaye rafiki, Ndiye mwema,
ndiye mwema. Damu yake yanikomboa,
Kutoka mwovu na dhambi. Asikia ombi
daima, Ahadi ya taji anipa, Nitakayovikwa
kwa neema, Mwendo utakapokwisha.
- Katika neno ninaona, Wema wake,
Wema wake. Mnyenyekevu na mpole,
Ni mwema kupita wote, Ashinda wote
kwa ushujaa, Anastahili kusifiwa,
Nikiwa naye ninashinda, Juu ya adui zangu.
- Amelifuta deni langu, Limefutwa,
limefutwa. Na dhambi zangu ‘kaondoa,
Mzigo nimepumzishwa. Sasa ninapendwa na
Mungu, Navikwa uzuri wa Yesu,
Kwa hiyo ninamtolea, Sifa kwa kum-tukuza.
- Sasa naimba kwa furaha, Kwa furaha,
kwa furaha, Maana Mungu ameandaa,
Mahali pa kupumzika. Hazimo huzuni na
shida, Na kifo hakitaingia, bali uzima
wa milele. Amani haitakwisha.
- Na humo namwona Mwokozi, Nimpendaye,
Nimpendaye, Aliyemwaga damu yake,
Kipatanisho kwa wote. Na humo wimbo
utavuma, Moyo washikwa na furaha, Nayo
itabakia kwangu, Hata milele mbinguni.
Comments
Post a Comment