321 NJIA YOTE ANIONGOZA

1. Njia yote aniongoza, Sifa na shukrani!
Posho safarini napewa, Sifa kwa Yesu!


Haleluya, ninamsifu Yesu siku zote zangu
Kwa kuwa amenikomboa, Sifa kwa Yesu!


2. Yote nimepata kwa Yesu, Sifa na shukrani!
Anikaribisha mezani, Sifa kwa Yesu!


3. Hatarini ananilinda, Sifa na shukrani!
Mkono wake unanikinga, Sifa kwa Yesu!


4. Yesu hanisahau kamwe, Sifa na shukrani!
Hata Shetani anipinge, Sifa kwa Yesu!


5. Nimetengwa na ulimwengu, Sifa na shukrani!
Nimo kati’ ufalme wake, Sifa kwa Yesu!


6. Siri zote anieleza, Sifa na shukrani!
Daima ninashangilia, Sifa kwa Yesu!


Comments