4 USIKU KABLA YA KUTESWA

  1. Usiku kabla ya kuteswa Yesu,
    aliwakusanya wanafunzi, Alifahamu
    kwamba saa yake,Ya kutolewa inakaribia


  2. Kwa roho aliona Gethsemane,
    Mateso yake, huzuni nyingi, Zaidi alihofu
    saa ile, Atakapoachwa hata na Mungu.


  3. Alitamani saa ya Pasaka, Pamoja
    nao wapendwa wake. Katika pendo lake
    kubwa sana, Aliyashinda majaribu yote.


  4. Akautwaa mkate, aka’mega: “Twaeni, mle,
    mwili wangu huu.” Na akawapa
    wanafunzi wake.Yu heri kila mtu ’aminiye.


  5. Baadaye akawapa na kikombe, akasema:
    “Nyweni nyote hiki! Ni damu yangu
    inayomwagika, Kwa ondoleo la makosa yote.”

Comments