51 NAONA AMANI GOLGOTHA


1. Jua la moyo wa kila Mkristo Ni Yesu
Naona amani Golgotha Alipojitoa Yesu
:/:Na huko nina kimbilio kwa Yesu Anipendaye.:/:


2. Sitaki ‘tamani fahari Na dhambi ulimwenguni
:/:Sababu wokovu ninao Katika damu yaYesu.:/:


3. Aliindoa kabisa Mizigo ya dhambi zangu.
:/:Na niliokoka hakika Kwa neno la Baba Mungu.:/:


4. Chakula cha rohoni mwetu Ni neno la Baba Mungu.
:/:Kinamletea Mkristo, Nguvu kwa safari Yake.:/:


5. Mimi ni hekalu la Roho, Anamiliki moyoni
:/:Kwa njia ya ahadi zake Yesu ananiongoza.:/:


6. Uliye dhambini ufike Kwa Yesu Mwokozi wako!
:/:Anakunyoshea mikono apenda kukupokea:/:


Comments