6 TWAMSIFU MUNGU DAIMA

  1. Twamsifu Mungu daima, Kwa damu takatifu,
    Inayotosha kutoa, Makosa yetu yote.


  2. Wakristo wakusanyika, Karibu na kisima,
    Hawapungukiwi kitu, Wakaa kwa Mwokozi.


  3. Tuimbe ulimwenguni, Juu ya upendo wake,
    Kwa kuwa twafunguliwa, Kisima cha Golgotha.


  4. Yesu Kristo ni kisima, Cha maji ya uzima,
    Wenye shida wastarehe, Waburudishwa kweli.


  5. Wenye dhambi wanaitwa, Kwa wingi wa
    rehema,Wakosaji na maskini, Wasaidiwa sana.


  6. Tumepata tunu kubwa, Neema kwa neema!
    Atakayeipokea, Ni mtu wa uheri.


  7. Haleluya! Twam-sifu Mwenyezi, Na Mwanawe
    Na Roho M-takatifu, Haleluya! Amina.

Comments