1. Mimi mgeni katika dunia, nasafiri kufika
mbinguni. Hata ikiwa hatari njiani, Nitashinda
pamoja na Mungu. Na kama Ibrahimu zamani,
Nitashinda kwa nguvu za Mungu. Nivumilie
nifike kule, Ndilo kusudi langu.
2. Nikitembea wakati wa giza, Nasaidiwa na
Bwana Yesu. Hata nikute mateso njiani,
Nakusudia kwenda mbinguni. Mungu ajua
mapito yangu, Naye Yesu atanifikisha.
Nivumilie nifike kule, Ndilo kusudi langu.
3. Tusisumbuke katika safari, Tuwatazame
walioanza. Yesu Mwokozi alitukomboa,
Msalabani alitufilia. Na atatufikisha mbinguni,
Twimbe kwa muda kitambo hivi: Tuvumilie
tufike kule, Ndilo kusudi letu.
Comments
Post a Comment