8 SIFA KWA YESU KRISTO

  1. Sifa kwa Yesu Kristo, Alichukua dhambi.
    Neema yatoka kwake, Ni kwa damu.
    Umeoshwa moyoni, Umepewa uhuru,
    Umeondolewa dhambi kwa damu?


    Ni kwa damu, Ni kwa damu, Umeoshwa
    moyoni, Je, umekuwa safi? Ni kwa damu,
    Ni kwa damu, Utaondolewa dhambi kwa damu.



  2. Ukilia machozi, Dhambi haziondoki.
    Haki utaipokea kwa damu.
    Mambo yasumbuayo, Yesu ayaondoa
    Ukombozi wapewa Ni kwa damu.


  3. Je, utakapoitwa Arusini mwake juu,
    Umevikwa nguo safi kwa damu?
    Je, wajenga mwambani, U mzima
    moyoni, Unashinda kila saa kati’ damu?


  4. Sifa kwa Bwana Yesu, Aliyetoa damu.
    Kwa damu ya thamani tutashinda.
    Asubuhi ile kuu, Vita yamalizika,
    Tutaimba kwa shangwe juu ya damu.

Comments