1. Tumo njiani kwenda mbinguni, Yesu
Kristo ndiye kiongozi. Hata tukikuta
majaribu, TunamtazamaYesu.
Mbinguni hatutatanyika tena, Huko hakuna
dhambi wala shaka. Hatutayaona machozi
kamwe, Ni furaha milele. Wanatungoja huko,
Wanatungoja huko, Malaika wanangoja
mbinguni. Wanatungoja huko, Wanatungoja
huko, Wakisema: “Karibu”
2. Tutawaona watakatifu, Walioshinda
maovu huku, Na tutamwona Mwokozi
wetu, Tutafananishwa naye.
3. Je, wapenda kufika mbinguni?
Yesu ni njia, uzima, kweli. Njoni kwa
Yesu ameyaandaa makao huko mbinguni.
Comments
Post a Comment