1. Yesu, Yesu, Jina zuri, Wimbo wa malaika!
:/:Limekuwa ndani yangu Mto wa furaha tele.:/:
2. Jina lake kama nyota Lanionyesha njia.
:/:Kati’ majaribu yote Na shida ulimwenguni.:/:
3. Ni mikono ya upendo Ya kunikumbatia.
:/:Hapo ninalindwa vema Kama chombo bandarini:/:
4. Jina la Yesu Mwokozi, Ni wimbo safarini!
:/:Linaniletea raha, Toka nchi ya mbinguni:/:
Comments
Post a Comment